Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 10:26

Darzeni ya vijana wa Morocco wajaribu kuingia Uhispania


Vikosi vya usalama vya Uhispania vikiwa katika doria wakati wahamiaji wa Morocco wakikusanyika kwenye mpaka wa eneo la Uhispania la Ceuta, Jumatano, Mei 19, 2021.
Vikosi vya usalama vya Uhispania vikiwa katika doria wakati wahamiaji wa Morocco wakikusanyika kwenye mpaka wa eneo la Uhispania la Ceuta, Jumatano, Mei 19, 2021.

Kundi la Wamorocco waliingia katika eneo la Melilla nchini Uhispania usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili, kundi la haki za binadamu lilisema.

Kundi la Wamorocco waliingia katika eneo la Melilla nchini Uhispania usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili, kundi la haki za binadamu lilisema, kati ya darzeni kadhaa waliojaribu kuvuka katika moja ya mipaka miwili ya ardhi ya Umoja wa Ulaya na Afrika.

Darzeni ya vijana wa Morocco walijaribu kuvuka kuingia Melilla kutoka mji wa mpakani wa Nador siku ya mkesha wa Mwaka Mpya, Shirika la Haki za Kibinadamu la Morocco (AMDH) lilisema kwenye Twitter.

Watu kadhaa waliingia kwa mafanikio licha ya kuwepo kwa polisi katika eneo hilo ilisema taarifa ya shirika hilo katika eneo hilo la Uhispania.

Hakukuwa na uthibitisho wa haraka kutoka kwa mamlaka ya Morocco au Uhispania.

XS
SM
MD
LG