Amemshinda Hou Yu-ih, mgombea urais wa chama cha upinzani cha Kuomitanga, au KMT chenye uhusiano wa karibu na China, na mkuu wa zamani wa polisi, pamoja na Ko Wen-je, mgombea urais wa Taiwan People’s Party, ambaye alijaribu kukiwasilisha chama chake kama mbadala vya vyama viwili vikuu.
Katika hotuba yake, Lai amesema ushindi wake wa Jumamosi ni ushindi wa demokrasia ya jumuiya ya kimataifa. “Tunaiambia jumuiya ya kimataifa kwamba kati ya demokrasia na ubabe, tutasimaa upande wa demokrasia,” alikiamba chumba ambacho kilikuwa na zaidi ya waandishi wa habari 100 wa ndani na nje ya Taiwan.
Forum