Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 17:39

Canada kutoa zaidi ya dozi milioni moja za chanjo kwa nchi za Afrika


Chanjo ya Johnson & Johnson ya Covid-19, iliyotolewa na Marekani kupitia COVAX, ilipelekwa Cambodia Julai 30, 2021.
Chanjo ya Johnson & Johnson ya Covid-19, iliyotolewa na Marekani kupitia COVAX, ilipelekwa Cambodia Julai 30, 2021.

Canada itatoa zaidi ya dozi milioni 1.3 za chanjo ya AstraZeneca ya COVID-19 kwa nchi tatu za afrika

Canada itatoa zaidi ya dozi milioni 1.3 za chanjo ya AstraZeneca ya COVID-19 kwa nchi tatu za afrika kupitia kituo cha kutoa chanjo cha COVAX, ushirika wa kimataifa wa kutoa chanjo -GAVI ulieleza alhamisi.

Nigeria, Kenya na Niger zitapokea mgawo wa kwanza wa chanjo za COVID-19 siku ya Alhamisi, Ushirika huo wa kimataifa ulisema.

Kituo cha COVAX, kikiungwa mkono na Shirika la Afya Ulimwenguni na GAVI, kinakusudia kupeleka chanjo bilioni 2 kwa nchi zenye kipato cha chini ifikapo mwisho wa mwaka 2021.

XS
SM
MD
LG