Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 06:05

Burkina Faso: Rais wa zamani Compaoré afunguliwa mashtaka


Rais wa zamani wa Burkina Faso Blaise Compaoré
Rais wa zamani wa Burkina Faso Blaise Compaoré

Mahakama ya Burkina Faso Jumanne ilimfungulia mashtaka rais wa zamani Blaise Compaore akiwa hayupo, kuhusiana na mauaji ya mwaka 1987 ya rais wa wakati huo Thomas Sankara, moja ya mauaji mabaya kabisa katika historia ya baada ya uhuru wa Afrika.

Sankara, mwanamapinduzi ambaye alikua anafuata siasa za ki Marxist aliyekua anaitwa mara nyingi “ Che Guevara wa Afrika” aliuwawa wakati wa mapinduzi ya kijeshi yaliyoongozwa na rafiki yake wa zamani, Compaore.

Compaore aliiongoza Burkina Faso kwa kipindi cha miaka 27 kabla ya kuondolewa madarakani mwaka 2014 na kukimbilia nchini Ivory Coast, ambako inaaminika bado anaishi huko. Awali, alikanusha kuhusika katika kifo cha Sankara.

Jopo la kijeshi lilimfungulia mashtaka Compaore anayeshutumiwa kwa kula njama katika mauaji hayo, kuhatarisha usalama wa taifa, waraka wa mahakama umeonyesha.

-Imetayarishwa na Patrick Nduwimana, VOA, Washington DC.

XS
SM
MD
LG