Wanachunguza vurugu dhidi ya serikali mwishoni mwa juma ambazo ziliharibu vibaya majengo ya umma katika maandamano dhidi ya Rais mpya Luiz Inacio Lula da Silva.
Wafungwa hao walikuwa wamekaa katika kambi moja ya mjini Brazilia iliyobomolewa na wanajeshi Jumatatu, siku moja baada ya mamia ya waandamanaji kuondoka kwenye kambi hiyo na kuvamia majengo ya Bunge la Brazil, Mahakama ya Juu na Ikulu.
Waandamanaji walitoa wito wa mapinduzi ya kijeshi ili kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa Oktoba ambapo Lula wa mrengo wa kushoto alimshinda kwa kura kidogo Bolsonaro.
Jaji wa Mahakama ya juu Alexandre de Moraes aliapa katika hotuba kupambana na “magaidi”.
Takriban waandamanaji 200 walikamatwa na kuzuiliwa gerezani kwa kuhusika kwao katika uvamizi wa Jumapili.
“Demokrasia itashinda na taasisi za Brazil hazitakuwa dhaifu,” Moraes alisema wakati wa kuapishwa kwa mkuu mpya wa polisi wa serikali kuu.