Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 25, 2025 Local time: 08:34

Boakai kutadhmini upya mikataba ya madini ya Liberia


Rais mteule wa Liberia Joseph Boakai
Rais mteule wa Liberia Joseph Boakai

Rais mteule wa Liberia Joseph Boakai aliyemshinda rais George Weah kwenye uchaguzi wa marudio wa Novemba 14 amesema kwamba utawala wake utatathmini upya mikataba ya uchimbaji madini, ili kuhakikisha inanufaisha nchi.

Boakai mwenye umri wa miaka 78, aliyewahi kuwa makamu wa rais alishindwa na Weah kwenye uchaguzi wa marudio wa 2017, alifanya kampeni kwa ahadi za kuiokoa Liberia, na aliiambia Reuters Jumapili kwamba anatarajia kukumbana na changamoto nyingi, hasa kwenye sekta ya uchumi.

“Hatua ya kwanza ya kuiokoa Liberia ni kuitoa mokoni mwa watu hawa,” amesema Boakai. “La pili ni kukabiliana na changamoto ambazo zimekuwa zikilikabili taifa hilo,” Boakai amesema, akiangazia ufisadi na ukosefu wa huduma za msingi.

Forum

XS
SM
MD
LG