Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Septemba 26, 2023 Local time: 05:36

Blinken aahidi msaada zaidi kwa Ukraine


Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken, kulia, na mwenzake wa Qatar Sheikh Maohammed bin Abdulrahman Al-Thani mjini Doha kwenye picha ya maktaba. Nov 22, 2022

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken  Jumanne anatarajiwa kutangaza msaada kwa Ukraine, ili kukarabati mifumo ya umeme iliyoharibiwa na mashambulizi ya Russia.

Tangazo hilo limetolewa pembeni mwa mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa wanachama wa NATO huko nchini Romania. Maafisa wa ngazi ya juu wa Marekani wamesema kwamba msaada huo utakuwa wa kutosha bila kutoa maelezo zaidi juu ya kiwango na hali ya msaada wenyewe.

Marekani pia inatarajiwa kuwarai washirika wengine wa Ukraine, kuepuka tatizo la umeme ambao ni muhimu zaidi wakati huu msimu wa baridi kali unapoanza. Wakati huo huo katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg Jumanne kwenye kikao hicho cha mawaziri cha siku mbili amesema kwamba muungano huo utaendelea kusimama na Ukraine,

XS
SM
MD
LG