Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 17, 2025 Local time: 17:08

China yaendelea kukabiliana na mlipuko mpya wa Covid-19


Mojawapo ya barabara zilizofungwa mjini Beijing kufuatia kuenea kwa maambukizi ya Covid-19
Mojawapo ya barabara zilizofungwa mjini Beijing kufuatia kuenea kwa maambukizi ya Covid-19

Mjii mkuu wa China wa Beijing Jumatatu umeongeza masharti ya kukabiliana na mlipuko mpya wa maambulizi ya Covid-19 kwa kufunga baadhi ya barabara pamoja na kuongeza vituo vya upimaji wa umma kwa wakazi wake.

Wakazi kutoka kwenye maeneo yaliyoathiriwa zaidi wameshauriwa kufanyia kazi nyumbani wakati barabara kadhaa pamoja na bustani zilkifungwa katika mji huo wenye takriban wakazi milioni 22.

Mlipuko wa sasa unasemekana kuwa mbaya zaidi kuwahi kutokea tangu kesi ya kwanza kugundulika mwaka 2020. Usafiri wa mabasi umesitishwa kwenye baadhi ya vitongoji kama vile Chaoyang na Fangshan ambavyo vinasemekana kuathiriwa zaidi. Kesi mpya 49 zimeripotiwa Jumapili na hivyo kufikisha jumla ya maambukizi mapya tangu Aprili 22 kufikia zaidi ya 760.

XS
SM
MD
LG