Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 22, 2025 Local time: 01:49

Baadhi wa Waebrania weusi wakabiliwa na tishio la kufukuzwa kutoka Israel


Msichana kutoka kundi la Waebrania weusi wa Israel kutoka mji wa kusini wa Dimona.
Msichana kutoka kundi la Waebrania weusi wa Israel kutoka mji wa kusini wa Dimona.

Waebrania  wa Israel wenye asili ya kifarika wanaoishi Jerusalem waliingia nchini humo kutoka Marekani kwenye miaka ya 60, lakini sasa baadhi yao wanakabiliwa na tishio la kufurushwa kutoka nchini humo.

Waebrania weusi kama wanavyojulikana kwa kawaida hawajichukulii kuwa wayahudi, ingawa wanadai kuwa na historia ya taifa hilo. Kwa miongo kadhaa wamekuwa wakiingia Israel, baadhi wakipewa haki za kuwa raia au vibali vya wakazi wa kudumu.

Hata hivyo 130 miongoni mwao hawana stakabadhi, na wameamrishwa kuondoka na serikali ya Israel. Takriban waebrania weusi 3,000 wanaishi kwenye miji iliyopo kusini mwa Israel, kitovu chao kikiwa mji wa Village of Peace ambao una majengo mafupi, na uliozungukwa na mimea na bustani.

Forum

XS
SM
MD
LG