Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Januari 14, 2025 Local time: 09:08

Angola yajiondoa kwenye Shirika la OPEC


Nembo ya Shirika la mataifa yanayoza.lisha mafuta , OPEC
Nembo ya Shirika la mataifa yanayoza.lisha mafuta , OPEC

Waziri wa Mafuta wa Angola ametangaza Alhamisi kwamba taifa hilo la Afrika Magharibi limefikia maamuzi ya kujiondoa kwenye Shirika la mataifa yanayozalisha Mafuta la OPEC.

Shirika la habari la serikali la Angop limeripoti kuwa waziri Diamantino de Azevedo, ametoa tangazo hilo kufuatia mkutano wa baraza la mawaziri, ukiongozwa na rais Joao Laurenco.

Baada ya tangazo hilo, Azevedo amewaambia wanahabari kwamba, “ Tunahisi kwamba kwa sasa Angola hainufaiki kwa kubaki kwenye shirika hilo, na kwa ajili ya maslahi yake, imeamua kujiondoa.”

Ripoti za vyombo vya habari zinasema kwamba huenda hatua hiyo imetokana na uamuzi wa OPEC mwezi uliopita wa kushusha kiwango cha mgao wa mafuta kwa Angola mwaka ujao hadi mapipa milioni 1.11 kwa siku, hatua ambayo haikubaliani nayo.

Inasemekana kwamba waziri huyo aliandikia OPEC barua ya kupinga hatua hiyo. Data iliyotolewa awali inaonyesha kwamba kufikia Oktoba, Angola ilikuwa inazalisha takriban mapipa milioni 1.6 ya mafuta kila siku.

Forum

XS
SM
MD
LG