Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 09:12

Al-Shabab huwenda ikashambulia tenka za mafuta Uganda


Lori zinazo safirisha mafuta na gesi nje ya kiwanda cha mafuta nje ya Nairobi, Kenya
Lori zinazo safirisha mafuta na gesi nje ya kiwanda cha mafuta nje ya Nairobi, Kenya
Polisi wa Uganda wameimarisha usalama baada ya kupokea habari za kijasusi kwamba wanamgambo wa Al-Shabaab wanapanga kuishambulia malori yanayosafirisha mafuta.

Al-Shabaab mara kwa mara imekuwa ikionya kwamba itaishambulia Uganda kwa sababu ina majeshi yake nchini Somalia kulinda usalama.

Wanamgambo wa Al-shabaab waliishambulia Uganda mwaka wa 2010. Takriban watu 76 waliokuwa wamekusanyika kwenye uwanja wa Raga wa Kyadondo kutizama fainali za Kombe la Dunia waliyapoteza maisha yao baada ya mabomu mawili kulipuka.

Tokea wakati huo, kundi la Al-Shabaab limekuwa likitishia kuzishambulia nchi zote ambazo zimeyatuma majeshi yake nchini Somalia kulinda usalama chini ya mwavuli wa Umoja wa Afrika. Uganda ndio iliyokuwa nchi ya kwanza kutuma majeshi mwaka wa 2007.
please wait

No media source currently available

0:00 0:02:53 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Baada ya kupokea taarifa kwamba huenda Al-Shabaab ikayashambulia magari yanayosafirisha mafuta, polisi imeanza kuyashindikiza magari ya mafuta yanayoingia nchini Uganda. Wanayazindikisha kutoka kwenye mipaka ya Kenya na Uganda ya Busia na Malaba.

Siku ya Jumanne, polisi ilifanya kikao na wafanyibiashara wanaosafirisha mafuta kuwaelezea hatua ambazo wamezichukua. Kila mfanyibiashara anafaa sasa kuipa polisi jina la dereva wake na nambari ya gari anayoiendesha. Ikizingatiwa kuwa wanamgambo huwa wajanja na wanaweza kuwatuma watu wao kuomba kazi kama madereva wa magari ya mafuta, polisi itafanyaje kuhakikisha kwamba madereva wanaowasajili sio magaidi.

Waganda wamekuwa na uoga kwamba bei ya mafuta huenda ikapanda ikiwa gharama ya polisi ya kuyazindikisha magari ya mafuta italipwa na wafanyibiashara wanayoyamiliki magari haya. Polisi imesema wao ndio watakaogharamika kwa hivyo bei ya mafuta itabakie ilivyo sasa.

Polisi inasema itaendelea kuyashindikiza magari ya mafuta hadi pale watakapopata taarifa kwamba hamna tisho tena la kushambuliwa hata kama ni miaka mitatu kutoka leo.
XS
SM
MD
LG