Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 00:35

Afrika lazima ibuni mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa-Bongo


Rais wa Gabon Ali Bongho akiwa na Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa mataifa Ban Ki Moon kwenye mkutano wa baraza la usalama la Umoja wa mataifa mjini New York, Juni 7, 2011,
Rais wa Gabon Ali Bongho akiwa na Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa mataifa Ban Ki Moon kwenye mkutano wa baraza la usalama la Umoja wa mataifa mjini New York, Juni 7, 2011,

Maafisa na wataalamu wa Afrika wanapaswa kunoa misimamo watakayowasilisha katika mkutano wa 27 wa kila mwaka wa Umoja wa Mataifa wa hali ya hewa utakaofanyika nchini Misri mwezi Novemba, alisema Bongo.

Mkutano wa tatu wa hali ya hewa barani Afrika unawakutanisha pamoja maafisa wa serikali na wadau zaidi ya 1,000 katika mji mkuu wa Gabon Libreville. Wanafanya kazi kutayarisha majibu madhubuti ya hali ya hewa ya kikanda barani Afrika.

Mabadiliko ya hali ya hewa ni changamoto kubwa barani Afrika ya wakati wetu, ikikuza ukosefu wa usawa wa kijamii, kisiasa na kiuchumi uliopo, Patricia Scotland, Katibu Mkuu wa taasisi ya Jumuiya ya Madola ya makoloni ya zamani ya Uingereza, alisema kwenye mkutano huo.

XS
SM
MD
LG