Haifahamiki sekta ya kifedha ya Taliban ambayo ina mzigo mkubwa kutokana na vikwazo hivyo imeweza vipi kufanya malipo makubwa ya mafuta kwa Russia.
Vikwazo vya kimataifa vimedumaza biashara za benki na Afghamistan, tangu Taliban ilipochukua udhibiti wa taifa hilo 2021. Marekani hata hivyo ilitoa mwanya wa kuendelea kutolewa kwa misaada ya kibinadamu, mradi isiwe inanufaisha viongozi wa Taliban na makampuni yao.
Mwaka uliopita, maafisa wa Taliban waliingia kwenye makubaliano na Russia ya kuagiza tani milioni 1 za petroli, milioni 1 za dizeli na nusu milioni za gesi ya kupikia. Licha ya kuwa Taliban na Russia wamewekewa vikwazo tofauti na mataifa ya magharibi, hakuna kinachowazuia kufanya biashara pamoja.
Forum