Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 27, 2025 Local time: 02:25

AFDB yaidhinisha mpango wa dola bilioni 1.5 kuisaidia Afrika kukabiliana na athari za vita vya Ukraine


Rais wa Benki ya Afrika kwa ajili ya maendeleo (AFDB), Akinwumi Ayodeji Adesina. Picha ya Reuters
Rais wa Benki ya Afrika kwa ajili ya maendeleo (AFDB), Akinwumi Ayodeji Adesina. Picha ya Reuters

Benki ya Afrika kwa ajili ya maendeleo( AFDB) imeidhinisha mpango wa dharura wa dola bilioni 1.5 ili kupunguza athari mbaya za ukosefu wa usalama wa chakula kutokana na vita vya Ukraine, mkurugenzi wa Benki hiyo amesema Jumatatu.

Takriban wakulima milioni 20 kwenye bara la Afrika watanufaika na mfuko huo wakati Afrika inakabiliwa na uhaba wa takriban tani milioni 30 za chakula, haswa ngano, mahindi na soya vinavyoagizwa kutoka Russia na Ukraine.

“Dola hizo bilioni 1.5 zitatumiwa kuzisaidia nchi za Afrika kuzalisha chakula na kufanya hivo kwa haraka,” rais wa AFDB Akinwumi Adesina ameviambia vyombo vya habari kabla ya mkutano mkuu wa kila mwaka katika mji mkuu wa Ghana, Accra.

Mpango huo una lengo la kusaidia kuzalisha tani milioni 38 za chakula. Ni pamoja na tani milioni 11 za ngano, tani milioni 18 za mahindi, tani milioni 6 za mchele na tani milioni 2.5 za soya.

Mpango huo utatoa pia ufadhili na dhamana ya mikopo kwa ajili ya usambazaji mkubwa wa mbolea.

XS
SM
MD
LG