Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 08:54

Wadau wazungumzia bajeti Tanzania


Bajeti ya mwaka 2009/2010 nchini Tanzania imepokelewa kwa mawazo tofauti nchini humo wakizungumza na sauti ya Amerika mwenyekiti wa sekta binafsi Ester Mkuzu anasema kuwa amefurahishwa na serikali kuongeza bajeti yake kwenye sekta ya kilimo, pia amefurahia elimu na miundo mbinu kupewa kipaumbele na mikakati ya serikali kwa ujumla nao baadhi ya wawakilishi wa wannachi wakiwemo wabunge na madiwani ambao ni Azan Zungu na Salim Mwaking'inda walisema taifa lolote linalotaka kupiga vita umasikini lazima liwekeze kwenye elimu na ndio maana serikali imeongeza bajeti ya elimu naye Bw.Mwakig'inda alisema nchi zote duniani zikitaka kumkomboa mtu mwenye kipato cha chini uhakikishe anapata chakula kwa bei nafuu,hata hivyo anasema kuna waliopinga hatua ya serikali kuondoa misamaha ya kodi katika baadhi ya maeneo katika mashirika ya dini na yasiyo ya kiserikali.

XS
SM
MD
LG