Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 23, 2025 Local time: 23:26

Waziri mkuu wa Ethiopia aitembelea Somalia ili kuimarisha uhusiano wa mataifa hayo mawili.


Ethiopia na Somalia waimarisha uhusiano wao
please wait

No media source currently available

0:00 0:01:14 0:00

Ethiopia na Somalia waimarisha uhusiano wao

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amefanya ziara ya saa kadhaa mjini Mogadishu siku ya Alhamisi, kwa lengo la kuimarisha makubaliano dhaifu ya maridhiano kati ya nchi hizo mbili kufuatia ugomvi juu ya ushirikiano wake na jimbo lililojitenga la Somaliland.

Abiy alipokelewa na Rais Hassan Sheikh Mohamud na kuwa na mazungumzo yaliyohusu masuala ya amani na usalama, uchumi, diplomasia na uwezekano wa kushirikiana katika miradi ya pamoja na miundo mbinu.

Mivutano kati ya nchi hizo mbili ilizuka mwishoni mwa mwaka jana baada ya Ethiopia kufikia makubaliano na jimbo lililojitenga la Somaliland ili kupata njia ya kufika baharini.

Lakini Mogadishu na Addis Ababa zilifikia makubaliano ya kurudisha tena uhusiano wao wa kidiplomasia mwezi Januari kutokana na upatanishi wa Uturuki.

Katika taarifa ya pamoja baada ya mazunguzmo ya Alhamisi nchi hizo zimeleza kwamba ziara hiyo ilikuwa ni ya kuimarisha kuruidshwa tena ushirikiano kati ya majirani hao wawili.

Kufuatia kurudishwa kwa uhusiano huo hatma haijulikani tena ya mkataba wa Ethiopia na Somaliland.

Forum

XS
SM
MD
LG