Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 12:28

Tshisekedi aahidi kujibu vikali uvamizi dhidi ya mashariki mwa DRC


Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amelaani Jumuiya ya Kimataifa kwa "kutofanya chochote" kukabiliana na mapigano makali mashariki mwa nchi yake.

Akilihutubia taifa Jumatano usiku kufuatia kutekwa kwa mji mkubwa kabisa wa mashariki wa Goma, Rais Tshisekedi alionya kwamba "kuna hatari kwa vita kugeuka kuwa vya kikanda."

"Kimya chenu na kutochukua hatua ni tusi kwa DRC," alisema kiongozi huyo akiongeza kwamba, kusonga mbele kwa wapiganaji wanaoungwa mkono na Rwanda kunaweza kupelekea moja kwa moja vita katika ukanda wa Maziwa Makuu.

Tshisekedi amesema kwamba jibu kali la kijeshi na lililopangwa liko njiani dhidi ya magaidi hao na wafadhili wao, akilalamika juu ya jinsi hali ya usalama ilivyozorota huko mashariki.

Wapiganaji wa M23 wakiwashinikiza wamamluki kutoka Romania hadi mpaka wa Rwanda kutoka Goma.
Wapiganaji wa M23 wakiwashinikiza wamamluki kutoka Romania hadi mpaka wa Rwanda kutoka Goma.

Hotuba yake imetolewa baada ya wapiganaji wa kundi la M23 kuteka miji miwili katika jimbo la Kivu Kusini siku ya Jumatano kufuatana na afisa wa serikali aliyezungumza na AFP.

Wakazi na maafisa wa miji ya Kiniezire na Mukwidja wanasema wapiganaji wa M23 hawakukabiliwa na upinzani wowote wakati wa asubuhi walipoteka miji yao.

Majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini, yenye utajiri mkubwa wa madini yenye thamani ya juu ,yamekua kati kati ya vita vya karibu miaka 30 vinavyo husisha makundi kadhaa yenye silaha, mara nyingi yakiungwa mkono na nchi jirani za Rwanda Burundi na Uganda.

Forum

XS
SM
MD
LG