Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 06, 2024 Local time: 07:04

Rais wa Ukraine asema nchi yake ina nafasi ya ushindi dhidi ya Russia kwa msaada mpya wa silaha


Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akiwa na wanajeshi wa Ukraine mbele ya ishara ya barabara inayoashiria lango la eneo la Donetsk, katikati ya Russia. (Ofisi ya rais wa Ukraine / AFP).
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akiwa na wanajeshi wa Ukraine mbele ya ishara ya barabara inayoashiria lango la eneo la Donetsk, katikati ya Russia. (Ofisi ya rais wa Ukraine / AFP).

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy alisema Jumapili kwamba nchi yake ina nafasi ya ushindi dhidi ya Russia na msaada mpya wa silaha kwa wanajeshi wa Kyiv ambao unakaribia kuidhinishwa na Bunge la Marekani  na kuungwa mkono na Rais Joe Biden.

Baraza la Wawakilishi la Marekani likiwa dhidi ya upinzani wa upande wa mrengo wa kulia wa chama cha Republican walio wengi katika bunge hilo, walipiga kura Jumamosi kwa dola bilioni 60.8 kama msaada mpya wa kijeshi kwa Ukraine, huku Seneti ikitarajiwa kupitisha hatua hiyo wiki hii na kisha Biden kutia saini.

Nadhani msaada huu utaimarisha vikosi vya jeshi, natoa maombi ambayo tunahitaji sana, ambayo maelfu ya wanajeshi wanahitaji sana Zelenskyy aliambia kipindi cha Meet the Press cha NBC, akizungumza kupitia mkalimani.

Forum

XS
SM
MD
LG