Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 11:10

Netanyahu aahidi kuendeleza uhusiano na Riyadh


Kiongozi wa chama cha Likud Benjamin Netanyahu akiwasalimia wafuasi wake katika makao makuu ya chama chake wakati wa uchaguzi mkuu wa Israel mjini Jerusalem, Novemba 2, 2022.REUTERS.
Kiongozi wa chama cha Likud Benjamin Netanyahu akiwasalimia wafuasi wake katika makao makuu ya chama chake wakati wa uchaguzi mkuu wa Israel mjini Jerusalem, Novemba 2, 2022.REUTERS.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema Alhamisi  kwamba amefuatilia  hatua za kuchukua.

Kuleta mafanikio ya kidiplomasia na Saudi Arabia na Mshauri wa Usalama wa taifa wa White House Jake Sullivan.

Netanyahu ameahidi kuendeleza uhusiano rasmi na Riyadh baada ya kusaini mikataba ya kurejesha uhusiano wa kawaida na Umoja wa Falme za Kiarabu na Bahrain mwaka 2020, lakini Saudi Arabia imehusisha hatua hiyo na utatuzi wa mzozo wa Israel na Palestina.

Taarifa kutoka ofisi ya Netanyahu ilisema Sullivan na Netanyahu waliijadili Iran, pamoja na hatua zinazofuata za kuimarisha mikataba ya Abraham na kupanua eneo la amani kwa kusisitiza juu ya mafanikio na Saudi Arabia.

Majadiliano yao yalifuatiwa na mkutano kwa njia ya mtandao kati ya Sullivan na wenzake wa Israel, Emarati na Bahrain, ofisi ya Netanyahu ilisema.

Sullivan alipaswa kusisitiza dhamira ya Marekani ya suluhu ya mataifa mawili katika mzozo wa Israel na Palestina wakati wa ziara yake, msemaji wa usalama wa taifa wa White House John Kirby alisema.

Mazungumzo ya amani yaliyosimamiwa na Marekani yaliyolenga kuanzisha taifa la Palestina huko Ukingo wa Magharibi, Jerusalem Mashariki na Gaza yalivunjika mwaka 2014.

XS
SM
MD
LG