Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 13:46

Umoja wa Ulaya na Morocco zatia saini mkataba wa ubia wa nishati safi


Bendera za Umoja wa Ulaya zinapepea nje ya makao makuu ya Tume ya Umoja wa Ulaya mjini Brussels, Ubelgiji, Septemba 28, 2022. REUTERS.
Bendera za Umoja wa Ulaya zinapepea nje ya makao makuu ya Tume ya Umoja wa Ulaya mjini Brussels, Ubelgiji, Septemba 28, 2022. REUTERS.

Umoja wa Ulaya na Morocco Jumanne zilitia saini mkataba wa ubia wa nishati safi ambao wanatumai utaimarisha ushirikiano katika nishati mbadala.

Nchi hiyo ya Afrika Kaskazini yenye jua kali inatafuta kutoa njia mbadala kwa mataifa ya Ulaya yanayojaribu kujiondoa kwenye nishati ya mafuta, ambayo bei yake imepanda kufuatia uvamizi wa Russia nchini Ukraine.

Mkataba wa Jumanne, uliotiwa saini na naibu mkuu wa Tume ya Ulaya Frans Timmermans na mwanadiplomasia mkuu wa Morocco Nasser Bourita, ni wa kwanza wa aina yake, Timmermans alisema katika hafla ya kutia saini huko Rabat.

“Inalenga kuunda "ukuaji endelevu unaoakisi changamoto za leo", aliongeza.

Bourita alisema kuwa ukweli wa kutisha kimataifa umeonyesha, Ulaya na Afrika Kaskazini, kwamba linapokuja suala la nishati, ni yenye kutegemewa pekee ndiko kunakozingatiwa.

Matamshi hayo, dokezo kwa hatua ya Russia kukata usambazaji wa gesi kwenda Ulaya kwa tuhuma za kulipiza kisasi kwa vikwazo vya Magharibi, pia yanakuja baada ya nchi jirani ya Algeria kusitisha usambazaji wa gesi kwa Uhispania kupitia bomba linalopita katika ardhi ya Morocco.

XS
SM
MD
LG