Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 07:59

Karim Benzema ashinda tuzo ya Ballon d'Or


 Karim Benzema wa Real Madrid baada ya kushinda Ballon d'Or huko Chatelet Theatre, Paris, Ufaransa - Oktoba 17,2022.
REUTERS
Karim Benzema wa Real Madrid baada ya kushinda Ballon d'Or huko Chatelet Theatre, Paris, Ufaransa - Oktoba 17,2022. REUTERS

Mchezaji wa kimataifa wa soka Karim Benzema ameshinda tuzo ya Ballon d'Or kwa upande wa wanaume kwa mara ya kwanza baada ya msimu mzuri akiwa na timu ya Real Madrid na kunyakua taji la Ligi ya Mabingwa na ligi ya Uhispania.

Benzema, mwenye umri wa miaka 34, alikuwa na msimu wake bora zaidi kuwahi kutokea Madrid, akiwa mfungaji bora wa ligi ya Uhispania na Ligi ya Mabingwa.

Alifunga mabao 44 akiwa na Madrid, yakiwemo 15 katika mashindano makubwa ya Uropa, na kumfikia Raúl González kama mfungaji wa pili kwa wingi wa mabao katika klabu hiyo nyuma ya Cristiano Ronaldo. Naye mchezaji wa Uhispania Alexia Putellas alishinda Ballon d'Or kwa upande wa wanawake kwa mwaka wa pili mfululizo kufuatia msimu mwingine bora kabisa na timu ya Barcelona.

XS
SM
MD
LG