Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 03:49

Brazil imepiga kura kumpata kiongozi ajaye nchini humo


Rais wa Brazil Jair Bolsonaro (L) na mpinzani wake katika kinyang'anyiro cha urais Luis Inacio Lula da Silva. Oktoba 2, 2022
Rais wa Brazil Jair Bolsonaro (L) na mpinzani wake katika kinyang'anyiro cha urais Luis Inacio Lula da Silva. Oktoba 2, 2022

Raia wa Brazil walipiga kura siku ya Jumapili katika duru ya kwanza ya uchaguzi uliokumbwa na mgawanyiko mkubwa nchini mwao katika miongo kadhaa huku mrengo wa kushoto wa Luiz Inacio Lula da Silva ukitarajiwa kumshinda kiongozi aliye madarakani Jair Bolsonaro wa mrengo wa kulia.

Ukusanyaji wa maoni umemuonyesha Lula da Silva akiongoza kwa miezi kadhaa, lakini Bolsonaro ameashiria huenda akakataa kukubali kushindwa hali inayozua hofu ya mgogoro wa kitaasisi au ghasia za baada ya uchaguzi. Ujumbe uliobashiriwa kwenye sanamu ya Kristo Mkombozi wa Rio de Janeiro ulisomeka kabla ya kura hiyo: "Amani katika Uchaguzi."

Tafiti nyingi zinampendelea Lula, ambaye alikuwa rais kutoka 2003 hadi 2010, kwa asilimia 10-15. Ikiwa atashinda zaidi ya asilimia 50 ya kura halali, ambazo wakusanyaji maoni kadhaa wanaonyesha idadi hiyo inaweza kufikiwa, na hivyo kupata ushindi wa moja kwa moja, na kuacha kura ya duru ya pili.

XS
SM
MD
LG