Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 03:13

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye


Hassan Sheikh Mohamud, Rais wa zamani wa Somalia ambaye bunge nchini humo limemchagua tena kuiongoza Somalia
Hassan Sheikh Mohamud, Rais wa zamani wa Somalia ambaye bunge nchini humo limemchagua tena kuiongoza Somalia

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu.

Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu.

Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017.

XS
SM
MD
LG