Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 03:38

Maandamano mapya yameibuka Sudan yanapinga mapinduzi ya kijeshi


Waandamanaji nchini Sudan wakipinga mapinduzi ya kijeshi nchini humo
Waandamanaji nchini Sudan wakipinga mapinduzi ya kijeshi nchini humo

Maelfu ya raia wa Sudan waliandamana katika mji mkuu wa Khartoum na miji mingine siku ya Jumatano katika maandamano mapya ya kupinga mapinduzi ya kijeshi ya Oktoba ambayo yaliitumbukiza nchi hiyo ya kiafrika katika machafuko ya kisiasa na kuzidisha matatizo yake ya kiuchumi.

Ilikuwa ni juhudi za hivi karibuni za kuwashinikiza majenerali wanaotawala ambao mapinduzi yao yamesababisha maandamano ya kila siku ya mitaani kudai utawala wa kiraia.

Wakitoa wito kwa makundi yanayounga mkono demokrasia, waandamanaji hao waliandamana mjini Khartoum na mji pacha wa Omdurman, huku kukiwa na ulinzi mkali kuzunguka makazi ya rais ambayo yameshuhudia mapigano makali katika maandamano ya awali.

Kulikuwa pia na mikutano ya hadhara kwingineko, ikiwa ni pamoja na Qadarif na Port Sudan, katika eneo la mashariki na eneo lililoharibiwa na vita la Darfur, upande wa magharibi.

Picha kwenye mitandao ya kijamii iliyoambatana na taarifa za shirika la habari la Associated Press zinaonyesha vijana wakichoma moto matairi na kufunga barabara.

XS
SM
MD
LG