Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 19:28

Pfizer na BioNTech zasema chanjo yao inadhibiti kirusi cha Omicron


Watu wazima wakisubiri watoto wanaopata chanjo ya Pfizer ya Covid 19, Kathmandu, Nepal, Nov 23, 2021. Picha ya AP
Watu wazima wakisubiri watoto wanaopata chanjo ya Pfizer ya Covid 19, Kathmandu, Nepal, Nov 23, 2021. Picha ya AP

Makampuni ya BioNTech na Pfizer Jumatano yamesema chanjo yao ya covid 19 ilifanikiwa kudhibiti kirusi kipya cha Omicron baada ya dozi tatu katika majaribio kwenye maabara, na yataweza kutowa chanjo dhidi ya Omicron ifikapo Machi mwaka wa 2022 iwapo itahitajika.

Katika taarifa ya kwanza rasmi ya makampuni hayo ya kutengeza dawa kuhusu ufanisi wa chanjo yao dhidi ya Omicron, BioNTech na Pfizer zimesema dozi mbili hazikuonyesha ufanisi wa kutosha wa kudhibiti kirusi hicho, lakini dozi ya tatu imeongeza ufanisi wa kukabiliana na kirusi cha Omicron kwa asilimia 25.

Lakini kituo cha utafiti chenye makao yake Durban Afrika kusini, African Health Institute kinasema matokeo ya utafiti wake yameonyesha kwamba chanjo zilizopo dhidi ya corona, zina ufanisi mdogo wa kudhibiti kirusi cha Omicron.

XS
SM
MD
LG