Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 14:54

Mexico yashinikizwa kuwapa hifadhi wahamiaji wanaotaka kuingia Marekani


mhamiaji akipewa huduma ya kwanza baada ya kuumia mguu
mhamiaji akipewa huduma ya kwanza baada ya kuumia mguu

Kundi la karibu wahamiaji 1000 wanaotafuta hifadhi wameingia katika mji mkuu wa Mexico, huku serikali ikikabiliwa na shinkizo kutoka kwa umoja wa mataifa, kuwapa vibali vya uhamiaji hara iwezeikanavyo.

Kundi hilo la wahamiaji, wakiwemo raia kutoka nchi nane, walianza safari jumamosi kutoka mji wa kusini wa Tapachula, wakisema kwamba wanatka haki, uhuru na maslahi yao kutiliwa maanani.

Wahamiaji hao wamesafiri kwa mguu kwenye barabara kuu kutoka jimbo la Chiapas, kwa uangalizi wa maafisa wa usalama na ulinzi wa wahamiaji

Wana matumaini ya kuingia Marekani.

Wamekuwa Tapachula kwa mda wa miezi miwili ambapo maafisa wa uhamiaji na tume ya uhamiaji ya Mexico, wamewaambia kwamba hawawezi kuwasaidia kwa sababu ni wengi sana.

Msemaji wa umoja wa mataifa Stephane Dujarric amesema kwamba ni muhimu kwamba mamlaka wanastahili kutoa kifadhi kwa wahamiaji wanaoomba, kwa haraka sana.

Maelfu ya wahamiaji kutoka Amerika ya kati na Haiti, wanakokimbia umaskini na machafuko, wamewasili Mexico wakiwa na matumaini ya kuingia Marekani.

XS
SM
MD
LG