Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Juni 18, 2025 Local time: 15:08

Trump atishia 'Kuiangamiza kabisa' Korea Kaskazini


Rais Donald Trump akizungumza kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza
Rais Donald Trump akizungumza kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza

Akizungumza kwa mara ya kwanza kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN) Rais wa Marekani ametishia kuiangamiza Korea ya Kaskazini ikilazimika ili kulinda washirika wake wakuu.

Rais Donald Trump akimwita kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, "Rocket Man" amesema, kiongozi huyo yuko katika safari ya kujitoa muhanga na kusema, dhamira yake ya kuendelea kutengeneza silaha za nuklia na makombora ya masafa marefu kunatishia dunia nzima na kunaweza kusababisha maafa makubwa ya binadamu.

Balozi wa Korea ya Kaskazini alitoka nje ya ukumbi wa mkutano wa UN kabla ya Trump kuwasili na hakuna aliyekuwa kwenye kiti chake hadi hotuba ya dakika 42 ya Rais wa Marekani kumalizika.

Ukumbi wa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa New York
Ukumbi wa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa New York

Trump alikuwa pia amegadhibika alipoizungumzia Iran akieleza kuwa serikali ya nchi hiyo ni ya kimabavu na inajificha nyuma ya pazia kwa kutumia kisingizio cha demokrasia.

Aliwambia viongozi wenzake waliohudhuria kikao cha ufunguzi cha 72 siku ya Jumannne kwamba, serikali ya Tehran imetumia rasilmali zake muhimu kugharimia makundi ya kigaidi "yanayowauwa Waislamu na kushambulia majirani zake; mataifa yenye amani ya nchi za Kiarabu na Israeli."

Kiongozi wa Marekani alizungumzia pia maswala mengine ya dunia kuanzia vimbunga vya hivi karibuni hadi nadharia yake ya "Amerika Kwanza"

XS
SM
MD
LG