Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 13:10

Museveni Awashutumu Wapinzani Wake


Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, amedai kwamba wapinzani wake wakuu wana njama za kuharibu jeshi la Uganda na kutaka kumuondoa madarakani.

Bwana Museveni aliyazungumza hayo katika mkutano na wanahabari ambapo katika mkutano huo amewalenga Amama Mbabazi, na Kiiza Besigye.

Vilevile Rais Museveni katika shutuma zake alimtaja aliyekuwa kiongozi wa ujasusi katika jeshi la Uganda, Generali David Sejusa.

Amesisitiza kwamba aliwapa viongozi hao wa zamani wa serikali na jeshi la Uganda nafasi ya kutatua matatizo ya nchi na wakashindwa kuyatekeleza.

Amedai yale yanayozungumzwa na wapinzani wake ni porojo kwa wapiga kura wakiwa na lengo la kumuondoa madarakani kwa kulitumia jeshi.

Uganda itafanya uchaguzi wake mwakani mwezi Febuari, ambapo katika kiti cha urais, wamejitokeza wagombea wanane lakini vinara ni Rais Museveni mwenyeye, Kiiza Besigye na Amama Mbabazi.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:48 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

XS
SM
MD
LG