Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 16:54

Mkuu wa majeshi ya Burundi asalimika na watu saba wafariki


General Prime Nyongabo mkuu wa majeshi ya Burundi akiwasili uwanja wa ndege Baidoa Somalia
General Prime Nyongabo mkuu wa majeshi ya Burundi akiwasili uwanja wa ndege Baidoa Somalia

Mkuu wa majeshi ya Burundi Jenerali Prime Nyongabo, amenusurika kutokana na jaribio la mauwaji alipokua anaelekea kazini katika mji mkuu wa Bujumbura siku ya Ijuma.

Msemaji wa jeshi Kanali Gaspard Baratuza, amesema msafara wa jenerali ulishambuliwa na watu walokuwa na mavazi ya kijeshi watu sita wameuliwa katika shambulizi hilo wakiwemu walinzi watatu washambulizi wawili na raia moja.

please wait

No media source currently available

0:00 0:01:57 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Msemaji huyo amesema watu walopanga njama hiyo wanataka kusababisha mgawanyiko katika jeshi la mungano la taifa na kutoa wito kwa utulivu kote nchini.

Burundi imeshuhudia ghasia na mauwaji ya watu mbali mbali tangu mwezi April, pale Rais Pierre Nkurunziza kusema atagombania mhula wa tatu katika uchaguzi ambao hatimae alipata ushindi.

Mkuu mwengine wa jeshi, mshirika wa karibu wa rais wa Burundi, Jenerali Adolphe Nshimirimana aliuliwa mwezi uliyopita katika shambulizi kama hilo la Ijuma.

XS
SM
MD
LG