Asasi za kiraia nchini Tanzania zimezindua ilani ya uchaguzi ili kuhakikisha uchaguzi huo unakuwa huru na haki .Na mtandao wa watetezi wa haki za binadamu nchini (THRDC) uliratibu shughuli nzima ya upatikanaji wa ilani hiyo.
Onesmo Ole Nguruma ni mratibu wa mtandao wa watetezi wa haki za binadamu nchini Tanzania (THRDC) akizungumza na Sauti ya Amerika anasema umuhimu wa ilani hiyo yao ni kuwasaidia wananchi kuweza kuwauliza wanasiasa maswala yanayowahusu zaidi.
Na kwa upande wa wanasiasa, Ole Nguruma anasema wanaweza kuomba ridhaa ya wananchi juu ya usimamizi wa rasilmali za umaa.</p>