"Watu wengi wameshanga kumona Rais Pierre Nkurunziza kuendelea na uchaguzi wa bunge licha ya upinzani mkubwa na shinikizo kutoka Jumuia ya Kiamtaifa , amesema mwenyekiti wa zamani wa chama tawala cha Burundi CNDD-FDD, Hussein Radjabu.
Akizungumza na Sauti ya Amerika akiwa uhamishoni, juu ya uchaguzi wa bunge ulofanyika Jumatatu nchini Burundi, Bw. Radjabu anasema anadhani Rais Nkurunziza amekaidi wito wa kimataifa kwa sababu ya "matatizo yanayo tokana na mambo aliyoyatenda katika Taifa la Burundi, kuwepo na mauwaji ambayo warundi wamelalamikia na matiafa mengine lakini hakuonesha mwenendo wowote ili aweze kubadili hali hiyo." Zaidi ya hayo anasema kumekuwepo na uporaji mkubwa wa mali ya umaa.
Bw. Radjabu amepongeza juhudi za Umoja wa AfrikaJumuia ya Afrika Mashariki na Jumuia ya Kimataifa kwa ujumla katika kutafuta suluhisho na kumongoza Rais Nkurunziza kuliongoza taifa mahala linapobidi kuelekea. Ila anasema, kiongozi huyo amekata kusikilza ushauri wa mtu yeyote, na hivyo watu wasikate tamaa.