Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 14:33

Washindi wa Nobel wataka hatua zichukuliwe kuhakikisha usalama wa watoto.


Washindi wa nishani ya nOBEL Malala Yousafzai and Kailash Satyarthi wakiinua medali zao kwa furaha wakati wa hafka ya kupokea huko Oslo,Norway Dec. 10, 2014.
Washindi wa nishani ya nOBEL Malala Yousafzai and Kailash Satyarthi wakiinua medali zao kwa furaha wakati wa hafka ya kupokea huko Oslo,Norway Dec. 10, 2014.

Mwanaharakati wa elimu Malala Yousfzai na mwenzake wa kutetea haki za watoto kutoka India Kailash Satyarthi Jumatano wameandika historia wakikabidhiwa tuzo ya Amani ya ulimwengu mjini Oslo, Norway.

Malala ambaye ana umri wa miaka 17 ndiye mdogo sana kuwahi kupokea tuzo hiyo huku Satyathri akiwa mzaliwa wa kwanza wa India kupata tuzo hiyo. Wote wawili watagawana tuzo hiyo ya dola million1.1 na pamoja na kutoa hotuba kwenye hafla hiyo. Kabla ya sherehe kuanza, Malala aliwapa barua viongozi wa dunia akiwasihi waufanye mwaka wa 2015 kuwa salama na wenye haki kwa watoto.

Alisema kwamba ingawaje tuzo hii inaonyesha kwamba vizazi vinaweza kuitisha maisha mema kwa watoto ni lazima pia kuwa na hatua za kufanya kila mtoto akawa na uhakika wa maisha ya usoni.

XS
SM
MD
LG