Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 16:12

Kucheleweshwa kesi kunachangia mlundikano wa mahabusi: Jaji mkuu Tanzania.


Kikwete akihutubia bunge la Tanzania.
Kikwete akihutubia bunge la Tanzania.
Tanzania Jumatatu imeadhimisha siku ya sheria nchini humo huku changamoto kubwa ikiwa ni utoaji haki kwa wakati kutokana na matatizo yaliyopo kwenye mfumo wa mahakama nchini humo.

Kucheleweshwa kwa kesi bila sababu za msingi kunaochangia mlundikano wa mahabusu magerezani umekuwa chanzo cha malalamiko kutoka kwa wananchi na wadau mbali mbali wa sheria nchini Tanzania hali inayochangia vyombo hivyo vya kutoa haki kulalamikiwa.

Rais Jakaya Kikwete aliyeshiriki maadhimisho hayo ya siku ya sheria nchini humo pia alisisitiza suala hilo la utoaji haki kwa wakati huku akitumia fursa hiyo kusisitiza kwamba serikali itaendelea kuziwezesha mahakama nchini kwa kuziongezea bajeti, kupanua wigo wa ujenzi wa mahakama za mwanzo na wilaya na kuboresha majengo ya mahakama zilizopo pamoja na kuongeza rasilimali watu katika kuhakikisha vyombo hivyo vya kutoa haki vinatimiza wajibu wao kwa ukamilifu.

kwa upande wake Jaji mkuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman amesema pamoja na changamoto nyingi zinazoikabili sekta ya mahakama nchini, zikiwemo upungufu wa mahakimu na vitendea kazi, mahakama itaendelea kuboresha utaoji wa huduma baada ya kuanzisha mpango maalum ambapo kesi zote za jinai na madai zinatakiwa kumalizika katika kipindi cha miaka miwili kuanzia sasa

Kauli mbiu ya siku ya sheria nchini Tanzania ni utendaji wa haki kwa wakati umuhimu wa kuwashirikisha wadau.
XS
SM
MD
LG