Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 01, 2023 Local time: 16:25

Majeshi ya Mali yapambana na wanamgambo wa Ansar Dine.


Một tấm ảnh ghép từ 36.422 ảnh cá nhân được đưa lên mạng xã hội vào ngày / hoặc gần ngày Trái Đất. NASA đã hỏi người dân toàn thế giới câu hỏi &quot;Bạn hiện đang ở đâu trên Trái Đất?&quot; trên mạng xã hội và yêu cầu họ trả lời bằng một tấm hình tự chụp. Người dân khắp mọi châu lục từ 113 nước và đăng hình của mình lên cho bức ảnh Trái đất như được chụp từ không gian này.<br /> &nbsp;
Majeshi ya Mali yalipambana na wapiganaji wa kiislam wakati wanamgambo wakijaribu kwa mara ya pili wiki hii kuingia ndani zaidi kwenye maeneo yanayodhibitiwa na serikali ya Mali.
Afisa wa juu wa jeshi la Mali akiongea kwa kwa misingi ya kutotajwa jina ameiambia VOA kwamba mapigano hayo yalitokea katika mji wa Kona, ambao upo karibu na eneo linalodhibitiwa na serikali kati kati ya nchi.
Mwandishi wa VOA katika eneo linalodhibitiwa na wanamgambo karibu na mapigano alisema malori yaliojaa wapiganaji wa kiislam yaliondoka kuelekea uwanja wa mapambano baada ya ghasia kuripotiwa kumalizika jumatano usiku .
Msemaji wa Ansar Dine moja ya makundi yanayopambana na serikali alikataa kuielezea VOA juu ya mipango yao kama wataingia zaidi upande wa kusini.
Mpaka sasa jeshi limeweka wanamgambo wa kiislam nje kidogo ya Mopti, eneo lililo ngome ya serikali. Majeshi ya Mali yalipambana na wanamgambo katika eneo hilo wiki hii.
XS
SM
MD
LG