Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 01:15

Somalia ingali yahitaji msaada kutoka Jumuia ya Kimataifa: Mahiga


Rais anaeondoka madarakani Somalia Sharif Sheikh Ahmed akipongezwa na mjumbe maalum wa UM Augustine Mahiga
Rais anaeondoka madarakani Somalia Sharif Sheikh Ahmed akipongezwa na mjumbe maalum wa UM Augustine Mahiga
Rais mpya wa Somalia, Hassan Shiekh Mohamud anasiku thelathini ya kuteuwa serikali mpya inayotazamiwa kuwahusisha wajumbe kutoka Koo na sehemu mbali mbali za jamii.

Akizungumza na Sauti ya Amerika Mjumbe maalum wa Umoja wa Matiafa kwa ajili ya Somalia Balozi Augustine Mahiga amesema huu ni wakati muhimu kwani ni mara ya kwanza kwa Somalia kujipatia serikali isiyo ya mpito baada ya zaidi ya miaka 20.

Mahiga amesema "kiongozi mpya Bw. Mohamud ni mtu mwenye ujuzi na Wasomali wamempenda na wanamatarajio makubwa na ataleta mabadiliko na tofuati kubwa na hasa mageuzi katika mueleko katika nchi ya Somalia."
please wait

No media source currently available

0:00 0:05:55 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Akikubali kushindwa, rais anayeondoka, Ahmed Shariff, alisema kuwa huo ndio ulikuwa uchaguzi wa kwanza huru nchini Somalia kwa miaka 42 tangu Mohamed Siad Barre kuchukua mamlaka mwaka 1969.
XS
SM
MD
LG