
Wakazi wa Goma wakimbia baada ya mji wao kutekwa na wapiganaji wa M23

Polisi wa mji wa Goma wakusanyika katika uwanja wa michezo Goma siku ya pili baada ya M23 kuuteka mji huo

Wanajeshi wa serikali ya Kongo baada ya kushindwa na wapiganaji wa M23.

Wapiganaji wa M23 waingia Goma

Mwanajeshi wa DRC auliwa na M23

DRC M23 rebels in Rutshuru

DRC waasi wa M23 mitaani Goma

Wapiganaji wa M23 wawasili Goma

DRC waasi wa M23 wapiga doria Goma

Msemaji wa M23 Vianney Kazarama

Utulivu unaone3kama umerudi Goma Jumanne jioni

Wanajeshi wa serikali ya Kongo baada ya kushindwa nguvu na wapiganaji wa M23.
Wapiganaji wa kundi la waasi la M23 huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congolwamechukua udhibiti wa mji wa Goma, risasi na mizinga ilirindima kwenye mji huo tangu jana usiku ambapo serikali ya DRC ilidai bado inaudhibiti wa mji wa Goma.
Lakini mwandishi wa VOA aliyeko Goma anaripoti kuwa askari wa jeshi la serikali FARDC wameukimbia mji huo na waasi wameukamata mpaka uwanja wa ndege wa Goma na hivi sasa mji uko chini ya udhibiti wa waasi hao.
Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani tayari watu 60,000 wameshapoteza makazi yao na wengi wanakimbilia Bukavu.
Hata hivyo Jumanne wafanya kazi wa Umoja wa Mataifa MONUSCO na viongozi wa serikali ya Congo walibebwa kwa ndege za UN na kupelekwa Bukavu na wengine Kinshasa. Jeshi la kulinda amani la umoja wa mataifa limeonekana katika mji likiwa katika vifaru vyao.
Waasi wanashikilia kwa sasa radio ya serikali na Uwanja wa ndege pamoja na mipaka ya Rwanda na DRC.