Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel wa Iran aliyefungwa gerezani, Narges Mohammadi, anakabiliwa na kesi mpya kuhusu tuhuma alizotoa dhidi ya vikosi vya usalama kuwanyanyasa kingono wafungwa wa kike, familia yake ilisema Jumamosi.
Maafisa katika mji wa George nchini Afrika Kusini walisitisha shughuli ya kuwatafuta manusura, na miili zaidi, siku ya Ijumaa katika eneo la jengo lililoporomoka ambapo watu 33 walifariki.
Mafuriko makubwa yaliyotokana na mvua kubwa za msimu magharibi mwa Afghanistan yamesababisha vifo vya takriban watu 50 na wengine kadhaa hawajulikani walipo, afisa wa Taliban alisema Jumamosi, akiongeza kuwa idadi ya waliofariki ilitokana na ripoti za awali na huenda ikaongezeka.
EU na Marekani walielezea wasiwasi wao wiki hii kufuatia kukamatwa kwa waandishi, wachambuzi wa kisiasa na wanasheria.
Baraza la Katiba lililotangaza ushindi huo pia lilikataa ombi lililotolewa na Waziri Mkuu Succes Masra la kutaka kufutwa matokeo hayo.
Rais Zelenskyy alisafiri Alhamisi kwenda Kharkiv kukutana na maafisa wa kijeshi huku mashambulizi ya Russia yakifanyika katika mkoa huo.
Hii itaashiria mabadiliko ya haraka kuliko kesi nyingi zilizo katika mfumo wa uhamiaji Marekani zinazochukua muda mrefu
Balozi wa Afrika Kusini nchini Uholanzi amelisihi jopo la majaji 15 wa kimataifa kuiamuru Israel iondoke bila masharti huko Gaza.
Vikosi vya Israel mapema mwezi huu vilichukua udhibiti wa upande wa Gaza wa mpaka wa Rafah na Misri.
Rais Xi Jinping wa China alisifu uhusiano kati ya China na Russia Alhamisi, na kuahidi kuuimarisha, alipokuwa akimkaribisha Rais wa Russia Vladimir Putin kwa mazungumzo mjini Beijing.
Niger ambayo haina bahari mwaka jana ilizindua bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka kwenye kinu chake kupitia CNPC.
Tangazo hilo linakuja wakati wanajeshi wa Ukraine wakirejea kaskazini mashariki mwa nchi hiyo kufuatia mapigano
Pandisha zaidi