Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 03, 2024 Local time: 04:38

UN yaeleza mgogoro wa Sudan unasambaa kwa kasi na umevuka viwango vya kawaida


Wakimbizi wa Sudan wakitafuta hifadhi huko Chad.
Wakimbizi wa Sudan wakitafuta hifadhi huko Chad.

Umoja wa Mataifa unaeleza kuwa mgogoro wa Sudan ambao unasambaa kwa kasi – ikwemo balaa la njaa, maradhi na ukosefu wa  makazi unaashiria hivi sasa ni tishio la kuiangamiza nchi nzima.

Hayo ameyasema Mkuu wa masuala ya kibinadamu na mratibu wa misaada ya dharura Martin Griffiths katika taarifa yake mwishoni mwa wiki.

Martin Griffiths
Martin Griffiths

"Vita vizito vimeuharibu mji mkuu Khartoum na Darfur tangu kuanza katikati ya Aprili na sasa vimeenea huko Kordofan.

Vita nchini Sudan vinachochea hali ya dharura ya kibinadamu iliyovuka viwango vya kawaida," amesema Griffiths.

FILE - Wakazi wa Sudan waliolazimika kuhama makazi yao kutokana na kuongezeka mashambulizi wanatandika mablanketi kulalia na mahema ya dharura katika kiji cha Masteri Darfur magharibi Sudan, on Julai 30, 2020.
FILE - Wakazi wa Sudan waliolazimika kuhama makazi yao kutokana na kuongezeka mashambulizi wanatandika mablanketi kulalia na mahema ya dharura katika kiji cha Masteri Darfur magharibi Sudan, on Julai 30, 2020.

Kulingana na taarifa hiyo ya UN katika mji mkuu wa Kordofan Kusini, Kadugli, akiba ya chakula imemalizika, huku mapigano na vizuizi vya barabarani vikiwazuia wafanyakazi wa misaada kuwafikia watu wenye njaa.

Katika mji mkuu wa Kordofan Magharibi, El Fula, ofisi za misaada ya kibinadamu zimevamiwa na bidhaa zote kuibiwa, taarifa imeeleza.

Griffiths amesema kuwa: “Nina wasiwasi mkubwa pia kuhusu usalama wa raia katika Jimbo la Al Jazira, huku vita vikisogea karibu na eneo linalozalisha chakula cha nchi nzima nchini Sudan.”

Kadiri vita vinavyoendelea, ndivyo vinavyozidi kuleta athari mbaya zaidi.”

Taarifa hiyo pia imeeleza kuwa baadhi ya sehemu zimeishiwa chakula na maelfu ya watoto wana utapiamlo na wako hatarini kupoteza maisha iwapo hawatapata matibabu.

Kulingana na taarifa ya UN maradhi ya kuambukiza yanaenea, na kuhatarisha maisha ya watu, hususan wale ambao tayari wamedhoofika kutokana na utapiamlo.

Pia imeeleza kuwa maradhi ya surua, malaria, kifaduro, homa ya dengue na kuharisha yameripotiwa kote nchini. Watu wengi hawawezi kufikia huduma za afya.

Forum

XS
SM
MD
LG