Muziki wa kizazi kipya umetawaliwa na vijana wengi wa kiume nchini Tanzania lakini wasichana pia nao hawako nyuma na kati ya hao yupo Josephine Sospeter Mwaluko.
Josephine ambaye kwa jina la kisanii anajulikana kama Jozi ametoa kibao chake kiitwacho Nipo Nawe.
Alizungumza na Sauti ya Amerika juu ya nyimbo yake hiyo na changamoto alizonazo katika sekta ya muziki nchini humo.