Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 18, 2024 Local time: 22:30

Israel yajitetea mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu kuhusiana na vita vya Gaza


Baadhi ya majengo yalioharibiwa na Irael kwenye mashambulizi yake dhidi ya Gaza.
Baadhi ya majengo yalioharibiwa na Irael kwenye mashambulizi yake dhidi ya Gaza.

Israel ambayo inashutumiwa kutekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya wapalestina kwenye vita vya Gaza Ijumaa imejitetea mbele ya mahakama ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa mjini The Hague, siku moja baada ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, kudai kwamba mashitaka hayo ni ya ‘kinafik’.

Taifa la Isreal ambalo lilibuniwa baada ya mauaji ya wayahudi, limekanusha vikali shutuma zilizofikishwa kwenye mahakama hiyo na Afrika Kusini, ikiwa moja ya kesi kubwa zaidi kuwahi kufikishwa katika mahakama ya kimataifa, na kuvutia mtizamo wa kimataifa na waandamanji kutoka mirengo yote, nje ya jengo la mahakama hiyo.

Mawakili wa Afrika Kusini Alhamisi wameomba mahakama hiyo Alhamisi kuiamuru Israel isitishe mara moja operesheni zake za kijeshi katika eneo lililozingirwa la pwani ambalo ni makazi ya takriban wapalestina milioni 2.3. Uamuzi wa ombi hilo huenda ukachukua wiki kadhaa, ingawa kesi huenda itachukua miaka kukamilika.

Forum

XS
SM
MD
LG