Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 17, 2024 Local time: 12:57

Awamu ya pili ya kuondoka kwa wanajeshi wa Umoja wa Afrika Somalia yaanza


Wanajeshi wa UPDF waliopelekwa Somalia. Picha na LUIS TATO / AFP.
Wanajeshi wa UPDF waliopelekwa Somalia. Picha na LUIS TATO / AFP.

Mwaka jana, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kauli moja liliidhinisha Ujumbe mpya wa Mpito wa Umoja wa Afrika nchini Somalia, unaojulikana kama ATMIS, kuwasaidia Wasomali hadi majeshi yao yatakapowajibika kikamilifu kwa usalama wa nchi hiyo mwishoni mwa mwaka  2024.

Awamu ya pili ya kuondoka kwa wanajeshi wa Umoja wa Afrika kutoka Somalia imeanza, umoja huo ulisema Jumatatu. Kujiondoa huko kunafuatia ratiba ya kukabidhi shughuli za usalama kwa mamlaka ya nchi hiyo, ambayo inapambana na washirika wa al-Qaida katika eneo la Afrika Mashariki al-Shabab yenye makao yake Somalia.

Mwaka jana, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kauli moja liliidhinisha Ujumbe mpya wa Mpito wa Umoja wa Afrika nchini Somalia, unaojulikana kama ATMIS, kuwasaidia Wasomali hadi majeshi yao yatakapowajibika kikamilifu kwa usalama wa nchi hiyo mwishoni mwa mwaka 2024.

Ujumbe huo unalenga kuondoa takriban wanajeshi 3,000 zaidi ifikapo mwisho wa mwezi, kati ya kikosi cha awali cha wanajeshi 19,626 wa AU. Katika awamu ya kwanza, baadhi ya wanajeshi 2,000 wa AU kutoka mataifa mbalimbali wanachama waliondoka Somalia mwezi Juni, na kukabidhi kambi sita za uendeshaji.

Forum

XS
SM
MD
LG