Waandamanaji waliokasirishwa na jaribio la bwana Compaore la kubadilisha katiba ili kuongeza utawala wake wa miaka 27 walifanikiwa kumuondoa madarakani na kumlazimisha kukimbia nchi jirani ya Ivory Coast hapo mwaka 2014.
Wanajeshi wa kikosi maalumu cha ulinzi wa rais wakiongozwa na Jenerali Gilbert Diendere, mshauri mkuu wa Compaore waliwachukua mateka maafisa wa serikali ya mpito mwezi mmoja kabla ya uchaguzi wa mwaka uliofuata.
Jaribio lao la kuchukua madaraka kwa wiki moja lilishindwa baada ya kuuliwa watu 14 na zaidi yaw engine 250 kujeruhiwa. Jenerali huyo anashtakiwa kwa kutishia usalama wa taifa, kufanya mauaji na shambulio.
Akiwa kizimbani alikataa kusema chochote huku akikaribiana na waziri wa zamani wa mambo ya nchi za nje anayetuhumiwa kupanga njama hiyo ya jaribio la mapinduzi.