Wanafunzi Marekani wanaopinga vita vya Israel na Hamas wanaendeleza maandamano

Vyuo vikuu Marekani vinakabiliwa na ongezeko la maandamano wakipinga vita vya Israel na Hamas. FILE PHOTO:

Wakati huo huo Chuo Kikuu cha Columbia kinaendelea na mazungumzo na wale walio katika kambi ya wanafunzi wanaounga mkono Wapalestina

Wanafunzi wanaopinga vita vya Israel na Hamas katika vyuo vikuu kote nchini Marekani, baadhi yao wamepambana na polisi wa kutuliza ghasia, waliandamana leo Jumamosi na kuapa kuendelea na maandamano yao, huku vyuo kadhaa vikiwalaani marais wa vyuo vikuu ambao wamewaita maafisa wa polisi kuwaondoa waandamanaji.

Wakati Chuo Kikuu cha Columbia kinaendelea na mazungumzo na wale walio katika kambi ya wanafunzi wanaounga mkono Wapalestina katika chuo kikuu cha New York, seneti ya chuo kikuu ilipitisha azimio Ijumaa ambalo liliunda kikosi kazi kuchunguza uongozi wa utawala, ambao wiki iliyopita uliwaita polisi katika jaribio la kuzima maandamano, na kusababisha vurugu na zaidi ya 100 kukamatwa.