Wakulima wapata habari njema kutoka COP28

Wataalamu wa kilimo na hali ya hewa wanasema kuna habari njema kwa wakulima wadogo duniani baada ya kutolewa tamko lililoidhinishwa na viongozi 134 wa dunia wakati wa siku za ufunguzi wa mkutano wa ulimwengu wa mabadiliko ya hali ya hewa COP28, mjini Dubai, mwezi huu.

Katika kile kinachojulikana kama azimio la COP28 la UAE kuhusu kilimo endelevu, mifumo ya chakula endelevu, na hatua ya hali ya hewa, viongozi wamekusanya zaidi ya dola bilioni 2.5 kuanza kushughulikia masuala ya hali ya hewa yanayohusiana na kilimo, maafisa wa mkutano huo walitangaza.

Tamko hilo liliambatana na tangazo la mipango mingine kadhaa, ikijumuisha ushirikiano wa dola milioni 200 kati ya UAE mwenyeji wa mkutano huo na mfuko wa Bill na Melinda Gates kuelekea utafiti unaohusiana na kilimo.