UN yasema LGBT wananyanyaswa wakiwa jela

Mahad, aliebadili jinsia kwenye sherehe za kupatiana Tuzo Kampala, 2015.

Mchunguzi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya mateso Juan Mendez amebaini kuwa mashoga na watu waliobadilisha jinsia wako katika hatari ya kukumbwa na mateso au hata kutendewa vibaya hasa wakiwa kizuizini .

Your browser doesn’t support HTML5

UN-LGBT

Mendez anasema ''Makundi haya ya wafungwa yanakumbwa na mateso na vitendo vingine vibaya, kote wakiwa kizuizini na hata nje ya vizuizi. Kuna takriban mataifa 76 ulimwenguni ambayo yana sheria zinazopinga mahusiano ya watu wa jinsia moja hata iwe faraghani".