Uganda kuchunguza kampuni za China

Kampala Uganda.

Bunge la Uganda limeanza uchunguzi ndhidi ya makampuni kutoka China yanayofanya shughuli za ujenzi na ukarabati wa barabara nchini humo.

Bunge la Uganda limeanza uchunguzi ndhidi ya makampuni kutoka China yanayofanya shughuli za ujenzi na ukarabati wa barabara nchini humo. Hatua hiyo imechochewa na ugunduzi kuwa Serikali ya Uganda hulipa fedha kwa makampuni tofauti na yale yaliopata kandarasi.

Your browser doesn’t support HTML5

Uganda

Uchunguzi huo anaongozwa na kamati ya bunge inayoshughulikia miradi ya Serikali. Ripoti za awali kutoka kwa wabunge zilisema kwamba wanakandarasi walikuwa wanatumia majina ya makampuni yenye umaarufu na sifa kupata kandarasi kutoka kwa Serikali,lakini fedha zinapolipwa zinaingia kwa watu tofauti.