Trump amekiri anapoteza kura za wanawake

Mgombea urais m-Republican, Donald Trump katika kampeni huko Maine, Marekani.

Mgombea urais wa Republican, Donald Trump alikiri Jumapili kwamba anapoteza uungwaji mkono kutoka kwa wanawake lakini lawama zote anazitupia vyombo vya habari kwa kuwasikiliza wanawake ambao alisema wametoa shutuma za uongo zinazohusu ngono dhidi yake.

Trump aliandika kwenye ukurasa wa Tweeter kuwa uchunguzi wa maoni unaonesha kinyang’anyiro dhidi ya mpinzani wake wa chama cha Democratic, Hillary Clinton bado ni kikali lakini alisema amepoteza idadi kubwa ya kura za wanawake kutokana na matukio yalioandaliwa ambayo hayajawahi kutokea.

Mgombea huyo wa kiti cha rais kwa chama cha Republican alirudia madai yake kwamba vyombo vya habari vinamuangamiza katika juhudi zilizoandaliwa na kampeni ya Clinton kwa kuweka taarifa ambazo hazijawahi kutokea kuwa habari.