Uchaguzi wa Zanzibar wafutwa

Wagombea urais Zanzibar Seif Shariff Hamad na Rais Ali Mohamed Shein

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar imetangaza kufuta matokeo na uchaguzi mkuu wa Zanzibar kutokana na matatizo yaliyojitokeza katika uchaguzi huo.

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) Jecha Salum Jecha alitoa tangazo hilo kwa njia ya televisheni na taarifa iliyosema kulikuwa na matatizo ndani ya tume yenyewe na pia katika vituo vya kupigia kura.