Siku ya Mtoto wa Kike Duniani : UN yasema magumu yanayomkabili yameongezeka

Your browser doesn’t support HTML5

Dunia leo inaadhimisha siku ya kimataifa ya mtoto wa kike, katika kipindi ambacho kuna janga la Covid 19 na hali yauchumi imedorora na kuongeza zaidi changamoto kwa wasichana.
Umoja wa Matafa ambayo iliipitisha siku hii mwaka 2011 kuhamasisha haki za wasichana inasema magumu yanayowakabili wasichana yameongezeka kutokana na mzozo wa kiafya wa virusi vya corona katika nyanja za elimu, ndoa za mapema, manyanyaso majumbani na fursa za kiuchumi. Inakadiriwa wanawake na wasichana milioni 435 ifikapo mwaka ujao wataishi kwa chini yad ola moja na senti 90 kwa siku.