Ruto asema akishinda uchaguzi wakimbizi Kenya watahamishwa kwa hiari

Your browser doesn’t support HTML5

Naibu wa Rais wa Kenya, William Ruto, ambaye pia ni mgombea urais nchini humo, amesema kuwa iwapo atachaguliwa rais, atahakikisha kwamba mchakato wa kuwahamisha wakimbizi kutoka kambi za Kakuma na Dadaab, utafanyika kwa hiari.

Mchakato huo ameeleza kuwa utafuata makubaliano kati ya Kenya, Somalia na shirika la wakimbizi la Umoja wa Matiafa, UNHCR. Alizungumza na mwenzangu BMJ Muriithi Katika mahojiano maalum katika studio za idhaa hii ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika, hapa mjini Washington...